Showing posts with label Afya na Wabongo. Show all posts
Showing posts with label Afya na Wabongo. Show all posts

Thursday, 4 December 2014

WATANZANIA TUJIFUNZE KUWEKA AFYA MIKONONI, TUSISUBIRI KUDRA YA WAKUBWA AU MUNGU





 Miaka yote niliyosafiri na kuishi ughaibuni nimebaini siri moja  kuhusu afya. Wananchi wengi duniani hawaijali miili hadi wanapougua.  Zamani kidogo nilikuwa nikiongea na mganga wangu wa Kichina. Nilikwenda kuchomwa zile sindano zao zinazobandikwa sehemu mbalimbali mwilini na kuachwa zimesimama juu ya ngozi mithili ya mishale ya nungu nungu. Accupuncture (tamka “Akapan-kcha”), ndiyo jina lake la kitaalamu. Tiba hii iligunduliwa, kutafitiwa na kuendelezwa maelfu ya miaka kabla ya kuzaliwa Bwana Yesu Kristo na Mtume Muhammad SAW.   Kazi ya sindano hizi  ni kurekebisha na kusawazisha nguvu (au umeme) mwilini. Unapochomwa tatizo si maumivu. Haziumi kama sindano za Kizungu tulizozoea. Kinachochachafya ni vile Mchina anavyotafuta “njia sahihi.” Je, umewahi kushika waya wenye umeme? Unaukumbuka ule mstuko? Ukiwa mdogo, ndivyo  Accupuncture ilivyo. 
 Sindano za Kichina. Picha ya Mtandaoni
 

Thursday, 20 September 2012

OLIMPIKI YA VILEMA IMEMALIZIKA -TUJITAYARISHE KWA MICHEZO YA MADOLA GLASGOW 2014


Awamu ya pili ya michezo ya Olimpiki ilishamalizika  London. Tokea 1988, mashindano haya ya vilema yalifanywa sehemu mahsusi  ya Olimpiki kule Korea Kusini, ingawa tukio lilikubalika rasmi  Olimpiki, Roma, Italia, 1960 .
Zaharani Mwenemti akiwa na wahudumu waliojitolea Olimpiki...picha na F Macha

 Mwaka huu Tanzania iliwakalishwa na Zaharani  Mwenemti aliyeshiriki utupaji tufe (“shotput”) na kisahani (“discus”). Mwenemti aliongozana na kocha, John Ndumbaro(mwenye ulemavu wa mguu mmoja) maofisa wawili – mkuu wa msafara, Johnsoon Meela na afisa utawala, Iddi Kibwana- (pichani chini) wote pia walemavu wanaotumia viti vya magudurumu au fimbo kutembelea.

Nilipohudhuria mashindano haya katikati ya juma nilishangazwa na kiasi kikubwa cha watazamaji. Bidii na juhudi za wanamichezo walemavu inasisimua na ni somo kwetu wote.
Suala la michezo ya vilema duniani lilianzishwa na mganga wa upasuaji na mishipa ya fahamu, Profesa Ludwig Guttman mwaka 1948.

Profesa Guttman....aliyeanzisha na kupigania uwezo na maendeleo ya walemavu baada ya vita vikuu vya pili vya dunia...
<--more--!>