Showing posts with label Wazungu na Nazi. Show all posts
Showing posts with label Wazungu na Nazi. Show all posts

Tuesday, 7 June 2016

WIMBI KUBWA LA MATUMIZI YA NAZI NA MADAFU MAJUU







Zamani wakati nikikua tuliambiwa ukinywa  madafu utaota busha. Njoo sasa katika nazi na mapishi yake. Watoto wa kiume tulibezwa tulipokuna nazi. Nakumbuka enzi nikiishi kikapera Mwananyamala , Dar es Salaam nilitembelewa na dada fulani. Alipogonga mlango akanikuta nimekaa juu ya mbuzi nikikuna nazi hakustahimili.
“Freddy hebu uko...pisha nikusaidie.”
Ilikuwa miaka 40 iliyopita. Sina hakika kama leo mambo yamebadilika.