Zamani wakati nikikua
tuliambiwa ukinywa madafu utaota busha.
Njoo sasa katika nazi na mapishi yake. Watoto wa kiume tulibezwa tulipokuna
nazi. Nakumbuka enzi nikiishi kikapera Mwananyamala , Dar es Salaam
nilitembelewa na dada fulani. Alipogonga mlango akanikuta nimekaa juu ya mbuzi
nikikuna nazi hakustahimili.
“Freddy hebu uko...pisha nikusaidie.”
Ilikuwa miaka 40 iliyopita.
Sina hakika kama leo mambo yamebadilika.
