Showing posts with label Ukeketaji Ulaya. Show all posts
Showing posts with label Ukeketaji Ulaya. Show all posts

Sunday, 3 January 2016

BARUA YA WAZI KWA RAIS MAGUFULI KUTOKOMEZA KABISA UKEKETAJI TANZANIA





 Mpendwa Rais John Magufuli,

Kwanza nakutakia kheri za mwaka mpya wa 2016.
 Ninakupongeza kwa kuanza kazi yako kwa kishindo. Kishindo kinachowapa wananchi wetu matumaini. Mvumo unaoukupa sifa Afrika Mashariki nzima hadi kuwafanya wenzetu watuonee wivu.  Afrika nzima inatamani ingekuwa na viongozi kama wewe. Tunaoishi Ughaibuni tutaendelea kuwa mabalozi wako.
Leo mada yangu Mheshimiwa Rais ni suala la ukeketaji.
Wasichana waliokimbia kujihifadhi jumba la Mugumu, Mara. Picha ya Anthony Mayunga kupitia gazeti la Mwananchi.