Jumapili iliyopita wanawake
watatu wa Kihabeshi walishinda
mbio za Marathon hapa London. Zilishirikisha wakimbiaji 38,000, wengi wananchi wa kawaida ( wasio wanariadha wa kulipwa); mataifa mbalimbali. Baada ya ushindi “
wanariadha hawa wenye fahari” walipeperusha bendera rangi kijani, manjano na
nyekundu. Bendera hii ya Ethiopia iliyosanifiwa mwaka 1897 imekuwa kielelezo maarufu cha Umoja wa Waafrika na
watu weusi duniani zaidi ya miaka mia moja sasa. Wekundu ni nguvu na imani, kijani ardhi na
manjano, kanisa. Tufasili hili kifupi.
Mwanamuziki maarufu wa Reggae kutoka Ivory Coast, Alpha Blondy. Picha ya Reggae Ville.
