Showing posts with label Kufunga na Figo. Show all posts
Showing posts with label Kufunga na Figo. Show all posts

Sunday, 17 March 2019

MARADHI YA FIGO NA FAIDA ZA KUFUNGA KULA- 4



Maradhi ya figo yamezidi sana kwa watu weusi, seuze Watanzania.
 Majuma mawili yaliyopita tulimpoteza Mtanzania maarufu sana kwa ugonjwa huu. Ni muhimu kujadili kwanini figo linaendelea kuwa tatizo kubwa kwetu.
Makala tatu zilizopita zimeongelea ulaji wa Saladi, mazoezi na kufunga kama njia za kujali figo, ini, moyo, ubongo,nk. Tumeambiwa  matumizi HOLELA ya dawa za kuzuia maumivu  changia tatizo au pia fadhaa (“stress”) dhalilisha figo.
Wiki iliyopita tulikumbushana kuwa kufunga  si tu Ramadhani au Uislamu.Tulitazama faida zake ikiwepo kupunguza unene, maradhi, kuupumzisha mwili na uwezekano wa kuwa na maisha marefu.
Tulitazama aina ya kwanza ya ufungaji, yaani kunywa  maji ( kidogo kidogo kwa wastani wa saa 36-72).