Showing posts with label Brazil. Show all posts
Showing posts with label Brazil. Show all posts

Monday, 17 June 2013

WATOTO WETU WANAVYOANZA KUATHIRIKA NA HALI YA KISIASA NCHINI


Wakati n’naishi Brazili miaka 20 iliyopita moja ya woga mkubwa ulioenea ni hatari ya watoto wadogo mijini. Hatari gani?
Sikiliza ...
Siku moja Jumapili  n’natembea ufukwe maarufu wa Copacabana  jijini Rio De Janeiro. Hapa pana eneo kubwa sana la kuogelea, wanawake warembo, majumba ya starehe, migahawa, magari, minazi na starehe za kuotea tu paukwa pakawa. Jaribu kulinganisha ufukwe huu na Coco Beach , Dar es Salaam. Anzia pale kilima kinachoelekea barabara ya Chake Chake ongoza hadi Kivukoni penye wauza samaki na boti linalovusha watu. Sema badala ya hospitali ya Ocean Road na Ikulu sasa weka majumba hayo niliyozungumzia ya starehe na sehemu ndefu  sana maridadi za kufanya mazoezi na kuogelea.
Watalii walipahusudu. Na hii si yote- ufukwe  wa Copacabana umeunganika na  Ipanema na Leblon, bichi nyingine mashuhuri za jiji. Wabrazili husema Mwenyezi Mungu aliuumba ulimwengu mzima kwa siku sita, ile ya saba akakaa kitako akikamilisha Rio De Janeiro peke yake. Nilikua na tabia ya kwenda kuogelea  na kufanya mazoezi pale mara mbili tatu kwa juma.