Showing posts with label Vyoo vya Ulaya. Show all posts
Showing posts with label Vyoo vya Ulaya. Show all posts

Monday, 17 December 2012

JE WANAWAKE WAKITAKA KUKOJOA MAJIANI INAKUWAJE MAJUU?...


Tupo sebuleni kwa jirani yangu mmoja mwanamke. Katualika majirani kusherehekea siku ya kuzaliwa miaka themanini. Themanini nakwambia! Wanawe wawili wamewasili na wajukuu na vitukuu toka Australia na Afrika Kusini kushangilia siku hii maalum ya ajuza mcheshi, roho safi; kibibi anayependwa na kila mtu hapa mtaani ninapoishi London. 
Mama wa Kizungu na mwanae wakingojea kuvuka barabara kando ya basi la ghorofa London...picha na F Macha...

 Nyumba imetota baraka.  Harufu mbalimbali za makulaji zinazitesa pua. Vyakula vimetandazwa mezani. Viazi  Ulaya vya kuchemsha na kuoka vinavyotengeneza msosi maarufu uliovum buliwa na hawa hawa Waingereza unaojulikana kama Chips. Mboga mbichi safi za saladi, nyanya, matango, vitunguu, jibini (chizi), mikate ya kila sampuli, samaki  na kuku wa kukaanga. Kawaida karamu za Majuu hutenganisha walaji wa nyama na wasiokula nyama (Vegetarians).
<--more--!>